UISLAMU UNAPIGWA VITA NA FREEMASONS DUNIANI SABABU YAKE NINI? SOMA KWA MAKINI.



UISLAMU UNAPIGWA VITA NA FREEMASONS DUNIANI SABABU YAKE NINI?
SOMA KWA MAKINI..
Sababu yake ndugu msomaji ni kwamba, baada ya kumalizika kwa Vita Baridi (Cold War) 1990
duniani ambapo kitovu cha Mfumo wa Ukomunisti (USSR) kikasambaratika chini ya rais Mikhail
(Michael) Gorbachev wa Urusi kwa msingi kwamba yeye hakuwa mjamaa (mkomunisti) hivyo
akiwa madarakani akaibadili Urusi kuwa yenye uchumi wa kibepari (Kiliberali/ Soko Huria) na
kuachana na Ukomunisti ulioasisiwa na Baba wa Ukomunisti katika taifa hilo Bw. Lenin ambayechini ya uratibubu wake raia walimpindua Mfalme Tsar Nicolas, katika Mapinduzi ya Urusi ya1917 ambaye yeye Lenin alikuwa mfuasi wa falsafa ya Umarx (Marxism) ilioanzishwa naMwanafalsafa wa kijerumani Carl Marx (1818-1883) mnamo mwaka 1848
ambapo mafundisho yake yalitaka mgawanyo sawa wa pato la taifa kati ya tabaka la wafanyakazi na watawala na hatimaye wafanyakazi ndio washike hatamu ya kuongoza nchi na nyenzo zote kuuza uzalishaji (viwanda) vimilikiwe na Umma sio watu wachache binafsi (mabepari) .
Hivyo huko Ulaya, sera hii ilionekana kuwa suluhisho la makandamizi na unyonyaji wa
walionacho (haves) yaani mabepari dhidi ya masikini wasionacho (have-nots). Mabepari huko
Marekani wengi wao ndio freemasons kama vile bilionea Bill Gates.
Kwa hiyo kwa maana nyingine vita baridi ilikuwa ni vita kati ya wakomunisti na freemasons chiniya taifa ya kimasonia la Marekani, kwa hiyo ushindi wa ubepari dhidi ya Ukomunisti ni ushindiwa freemasons kusonga mbele ili kutaka kuitawala dunia yaani “New World Order” kwa Kilatiniwanaita “Novus Ordo Seclorum” ambayo alama yake ni ndege tai ambaye pia yupo katika notiya dola ya Marekani [57]. Watu wengi huziamini habari za kipropaganda za vyombo vya habarivya kimataifa kama vile BBC, VOA, RFI (Radio France International), CNN, RDW (Radio DeutchWelle) nk. bila ya kujua kuwa asilimia kubwa ya vyombo vya habari vya kimataifa vinamilikiwana Freemasons duniani kama nyenzo za kuhalalisha propaganda na Ushetani wao ikiwemoumagharibishaji (westernization) [58] ambao kwa lugha rasmi na ya mficho inaitwa Utandawazi
ambao aghalabu watu wengi hawajui kuwa ni propaganda sio uhalisia wa dhana hii.
Utandawazi si chochote bali ni Sera au mkakati danganyifu wa kipropaganda unaodaiwa eti
kukusudia kuleta maendeleo dunia nzima zikiwemo nchi masikini ziwe kama za Ulaya, sasa
kama ndio, mbona Ulaya pia masikini wapo hata ombaomba?! kwa nini wasingeanza huko?! huuni ulaghai mtupu, bali ukweli ni kwamba Utandawazi ni mkakati wa Mawakala wa Shetani
(freemasons) duniani waliouanzisha na kuutumia kama nyenzo ya kuupotosha ulimwengu ili
Umasonia kutawala dunia! ni pamoja na wao kujitajirisha zaidi, kuipotosha jamii kimaadili,
kifikra, kiuchumi kwa kuifukarisha jamii katika lindi la umasikini wa kutupwa [59] kwani mtu
akishakuwa masikini huwa aghalabu ni rahisi kumtumia au kumuendesha katika ‘ushenzi’ wa
kumuasi Mwenyezi Mungu namna watakavyo vile watakavyo wamasonia, hii ikiwa ni pamoja na
kubuni ajira za kumuasi Mungu eti ili watu uondokane na umasikini na lazima mtu utakubali,
mfano ni uhalalishwaji wa biashara za ngono huko Ulaya.
Ifahamike kwamba hata utamaduni ulioko sas huko Magharibi, sio utamaduni halisi wa mzungu
wa huko bali ni matokeo ya udhibiti wa Umasonia, kwa hiyo wamefanikiwa huko kwao sasa
wanaitaka dunia nzima.
Baada ya ya kumtokomeza adui yao huo Ukomunisti 1990, freemasons wakaona adui aliyebak ni Uislamu kama kikwazo kwa wao kuiharibu jamii duniani ikiwemo kushika kwao soko la mafutaduniani, kusambaza mfumo wa Riba duniani, kukua kwa Uislamu Magharibi, kuwa na msimamona maadili ya dini yakiwemo mavazi, ulevi, uzinzi na kila kinachopingana na Mungu, na uislamu
kuonekana kikwazo cha kukuwa kwa “Ushetani” (Freemasonry) duniani.
Kwa hiyo kuanzia 1992 kwa urasmi kabisa taifa la ki-freemason Marekani kwa kutumia Taasisi
yake ya kimasonia ya kimataifa, yaani Umoja wa Mataifa (UNO) ambayo wengi wanadhani ni
taasisi ya mataifa yote duniani kumbe sivyo ila mali ya wamasonia! Marekani ikaanza kwa
kuivamia Iraq (nchi ya pili kwa kuzalisha mafuta duniani) chini ya Sadam Hussein (Gulf War)
baada ya kumgombanisha na muislamu mwenzake wa Kuwait na kujifanya anakwenda
kumsaidia kumbe ni ‘wagawe ili uwatawale’ (Divide and Rule) na ndio maana 2003 wakaja na
vita ya pili ya Iraq kwa kusingizia eti Saddam anatengeneza silaha za nyuklia, ambazo
hazikupatikana mpaka leo!
na Sadamu akanyongwa kwa kukatwa kichwa siku ya Idd Kubwa ya
2003 na bado Marekani hadi sasa hataki kuondoka Iraq moja kwa moja, lengo ni ili andelee
kupata maslahi toka kwa vibaraka aliowapandikiza baada ya Saddam Hussein.
Freemasons wakati mwingine anapokuja unaweza kudhani ni mkristo kwa kuwa ni mmagharibi
jina lake lina asili ya kimagharibi kama vile la kigiriki, kilatini, kiingereza, kifaransa nk. kama lilivyochimbuko la ukristo wenyewe.
Kiuhalisia, Ukristo katu sio kikwazo dhidi ya kukua kwa U-freemason duniani kwani tayari freemasons wamefanikiwa kuudhibiti ukristo katika chimbuko au kitovu chake huko Ulaya ndani ya makanisa kiasi kwamba wanaupeleka kwa kuupindisha vile watakavyo kwani walishafanikiwa kujipenyeza katika kada mbalimbali za kanisa na uongozi wa
juu wa madhehebu mbalimbali duniani.
Na Freemasons wengine hata kuanzisha madhehebu au taasisi mbalimbali ndani ya makanisa
kufanikisha kuongoza kanisa kimasonia aghalabu bila ya waumini kujua wamasonia hao
wakijifanya kuwa viongozi wa kikristo, na kuweza kuhalalisha Ushetani kama vile ushoga, usagajina, uvaaji mavazi yasiostahili katika ibada ndani ya makanisa na mazingira kwa ujumla, kwamfano huko Uingereza katika Uanglikana na Marekani katika Usabato huko Marekani. MfanoAskofu Michael Ingham wa Dayosisi ya New Westminster huko Uingereza ameruhusu na
kubariki ndoa za jinsia moja!
Mfano Ignatius Loyola mwaka 1534 ndani ya kanisa la Roma alianzisha Shirikisho aliloliita
“Society of Jesus” au “Jesuits” yaani “Jamii au Watu wa Yesu” ambalo lilipata baraka za Papa
baada kuaminishwa kuwa eti Loyola aliunda shirikisho hilo ili kuulinda Ukatoliki dhidi ya harakati za zilizokuwa zimeibuka huko Ulaya Magharibi hasa Ujerumani, Uingereza, Uholanzi, Ufaransa.Hispania nk.
kujitenga na Ukatoliki na kuanzisha Uprotestanti chini ya Martin Luther.
Lakini kumbe ukweli ni kwamba kwa mujibu wa mtafiti wa kimarekani Robert Howard anasema
Bw. Ignatius Loyola alikuwa Freemason ambaye ndiye aliyeanzisha “Iluminati” nae akawa mkuu wa kundi hilo, yaani kundi la wanachama wa kimasonia wenye kuanzia daraja la 5 hadi la juu yaani la 33 ambalo ni tabaka la wamasonia linaloaminika kuwa lenye elimu kubwa ya kimasonia ambalo kwa kuanzia Loyola aliweka makao makuu huko Visiwani Malta ambao wanamwabuduShetani (Lucifer) . Pia kwa mujibu wa mtafiti Kareena Kapoo kupitia mtandao wa intaneti katika http://www.DesiHits.com/KareenaKapoor anasema kuwa Martin Luther alikuwa Freemason ambaye ndiye aliyeupinga Ukatoliki duniani na kuasisi Uprotestanti ambapo alianzisha kanisa  lake la dhehebu la Lutherani duniani.
Mfano mwingine wa namna gani freemasons wamefanikiwa sana kuingia katika makanisa
hatimaye kuliongoza katika misingi isiyo ya kibiblia ni pamoja na kuingiza misingi ya “Riba”
kutumika katika makanisa huko Ulaya na hata Tanzania kwa sasa na maeneo mengine ya dunia.
Je mpendwa msomaji! unaikumbuka Taasisi iliyojiita “DECI Tanzania” iliyokuwepo takriban kati
ya 2006-2010? ambayo iliingia Tanzania, chimbuko lake kwa yakini baadaye ikaja kufahamika ni
Marekani toka katika kanisa la Pentekoste! siri iliyotolewa na wachungaji wa kanisa hilo baada
ya kukamatwa na jeshi la polisi la Tanzania baada ya Serikali ya Tanzania kuipiga marufuku
taasisi hiyo ambayo watanzania walikuwa hawajui kuwa ni ya kimasonia toka Marekani! na
wengi “walipanda” pesa zao (waliweka) ili zizae “Riba” baada ya wiki kadhaa, hatimaye DECI
ilifungwa na kwa kuwa ilikuwa haikusajiliwa kufanya kazi za kibenki na hivyo watanzania wote
waliopanda pesa hawakupata walichoweka wala riba walikuwa wanaisubiri kwa matumaini na
shauku kubwa.
Miongoni mwa mambo ambayo freemasons walifanikiwa kwa mujibu wa mtafiti Robert
Howard katika makala yake iliyoitwa “United States Presidents and The Illuminati / Masonic
Power Structure, Hard Truth/Wake Up America” kupitia mtandao wa intaneti:
http://www.forbiddenknowledge.com ni kuuharibu ukristo moja wapo kama mfano na ushahidi ni kile
kinachoitwa “Apocrypha” ambapo mwaka 1776 tabaka la vyeo vya juu la kimasonia (Illuminati)
huko Ulaya liliunda kamati maalum ya kuiharibu Biblia ambayo iliitwa “The Biblical Destruction
Group” ambapo pamoja na mambo mengine, walifanya kile walichokiita ‘To Eliminate the
Opiate” (out of print)’ kamati hii ilikuwa chini ya mmasonia aitwae Rabbi Antelman na
ilifanyakazi kwa miaka 50 [62] na walifanikiwa kufikia 1826 kufuta maandiko (vitabu) 14 toka
kwenye Biblia na kisha kuchapishwa toleo la Biblia lililoitwa toleo la Mfalme James yaani “King
James Version” [63] inayotumika hadi sasa, na sasa wana mpango kufuta maandiko yoye
yanayoonekana kama yanamkandamiza mwanamke, mpango ambao ulianza kupangwa mwaka 1988.
Pia vita dhidi ya Uislamu ni pamoja na wao kuanzisha taasisi maalum za kupambana na Uislam
kama hii ya Jihad Watch chini ya Robert Spencer. Kuchochea vita kwa kupandikiza vibaraka
katika nchi za kiislamu kwa kisingizio cha Demokrasia mfano yaliyotokea Palestina (kwa
kuwapandikiza wayahudi tangu 1947 na kuitumia yao ya kimasonia ya Umoja wa Mataifa -UNO
kuasisi taifa la Israel ambalo halikuwepo ndani ya ardhi ya wapalestina mwaka 1967 baada ya
kuwasukumia huko Ukanda wa Gaza nk. na mpaka leo Wayahudi wakiendea kujenga makazi yakudumu katika ardhi ya Wapalestina). Na yale yanayotokea 2011-12 Libya, Misri, Algeria,
Tunisia na Syria ni mkakati wa kimasonia wa “wagawe ili uwatawale” na sasa wakiwa katika
mkakati dhidi ya Sudan kwa Omar Al-Bashir na Iran kwa Mohammed Nejad.
Demokrasia ya Kimagharibi sio demokrasia ya kweli kama watu wanavyodhani, kuiamini na
kuichukulia kwani huzingatia utashi wa wengi tu, je wale wachache wanachukuliwaje? zaidi ya
kupuuzwa hata kama waliowengi hawako sahihi kimantiki katika kuchagua kwao?! na hatakamakimantiki wachache wanasimamia uhalali na wengi wanasimamia udhalimu, hivyo kwa hali hiidhana ya “Demokrasia ya Magharibi ni Udikteta dhidi ya wachache” [64] si vinginevyo ikiwa ni moja ya nyezo ya njia wanayopitishia umasonia. Hivyo dhana ya Demokrasia ingelikuwa sahihi
kama ingezingatia ubora/ ufanisi wa mawazo ya wengi na wachache, sio uwingi wa waliochaguakwani hata wengi wanaweza kusimamia ujinga au udhalimu, fikra ya kwamba penye wengihapaharibiki neno haina nafasi katika eneo kama hili hili kwani kauli hii ni ya kubahatisha tu.Mfano mzuri ni Libya ambapo hapakuwa na Demokrasia ya kimagharibi lakini MuammarGaddaffi (1942-2011) aliyeingia madarakani Libya 1969 akiwa na umri wa miaka 27 kwamapinduzi ya kijeshi kwa kumng’oa Mfalme Idrisa wa I aliyekuwa akiwajali kimaslahi
wamagharibi huku akiacha kutumia rasili mali za mafuta za nchi hiyo kwa ajili ya wananchi wake.
Pamoja na kwamba Gaddaffi hakufuata Demokrasia bali utawala wa kijeshi, alitumia vema rasilimali za mafuta ya Libya kwa ajili ya wananchi wa nchi hiyo kuliko rais au dikteta yeyote duniankupata kutokea ambapo kila raia wake alipata huduma za msingi bure zikiwemo Elimu tokachekechea hadi viwango vyote katika elimu ya vyuo vikuu (yaani mtu asome atakavyo), hudumaya maji bure, umeme bure, nyumba bure na afya bure nk. Ni wapi duniani pameshawahikufanywa hivyo chini ya kiongozi gani?
Ikumbukwe pia Gaddaffi aliwahi kujitolea kugharamia mkutano wa Umoja wa Nchi za Afrika
(AU) uliowahi kufanyika Ethiopia, hii ni baada ya kuonekana mkutano huo usingefanyika kwa
ukosefu wa michango ya kifedha toka kwa nchi wanachama. Pia alitoa misaada mingi katika nchiza kiafrika ya kijamii na kiuchumi na mpaka anaondoka madarakani Libya haikuwa na denilinayodaiwa na taifa au benki yoyote duniani.
Waliosemekana eti waasi dhidi ya Ghadaffi ni wale wapinzani wa Ghaddaffi ambao waliokimbia
na kuishi uhamishoni kama vile Uingereza na hivyo wakatumika na wamasonia wa magharibi
kwa kupewa silaha na kusaidiana na majeshi ya kimagharibi ya NATO ili waje kuwa vibaraka
ambao nao sasa wamegawanyika, kuna wanaotaka serikali ya kidemokrasia, wengine ufalme nakwa upande wa wananchi wengine wanataka serikali ya kiislam, wakati waasi wote mwanzo
walidai Gaddaffi hakuwa na Demokrasia kwa hiyo walikuwa wanpigania Demokrasia.
Kipi kilicho bora, ni demokrasia katika maisha duni, au maisha bora nje ya demokrasia ya
kimagharibi? Tafakari! Ifahamike sipingi demokrasia bali ile ya kimagharibi ambayo ni njia ya
kupenyezea umasonia duniani. Dhana ambao ilianzishwa na mwanafalsafa wa kale wa kigiriki
Bw. Arristotle (300BC, mwanafunzi wa Plato) na kuja kuendelezwa kisasa zaidi na wanafalsafa
wa falsafa ya Sheria yaani Jurisprudence wafaransa aliyeitwa Montesquieu na Jean Jacques
Rousseau katika karne ya 17-18…HILI SI LA UISLAMU TU HATA NYINYI WAFUASI WA KRISTO LINAWAHUSU..”NEW WORLD ORDER”

Share on Google Plus

About DAIMA ANGAZA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

1 comments:

  1. Kipi kilicho bora, ni demokrasia katika maisha duni, au maisha bora nje ya demokrasia ya
    kimagharibi? Tafakari! Ifahamike sipingi demokrasia bali ile ya kimagharibi ambayo ni njia ya
    kupenyezea umasonia duniani. Dhana ambao ilianzishwa na mwanafalsafa wa kale wa kigiriki
    Bw. Arristotle (300BC, mwanafunzi wa Plato) na kuja kuendelezwa kisasa zaidi na wanafalsafa
    wa falsafa ya Sheria yaani Jurisprudence wafaransa aliyeitwa Montesquieu na Jean Jacques
    Rousseau katika karne ya 17-18…HILI SI LA UISLAMU TU HATA NYINYI WAFUASI WA KRISTO LINAWAHUSU..”NEW WORLD ORDER

    ReplyDelete