26 Swafar 1438 H | |
Jiunge Upokee Jarida La AlhidaayaUser login |
Madhara Ya Kufuata Matamanio
Shaykh Swaalih Aal Twaalib
5, Rabiy'ul Aakhir 1426 (13, May 2005)
Imetarjumiwa na Ummu Ummu Ayman
Shukurani zote Anastahiki Allaah, Mola wa ulimwengu wote. Rehma na amani zimshukie Mtume (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam), ahli zake na Masahaba wake.
Enyi Waislamu muogopeni Allaah kwa kadri Anavyopaswa kuogopewa. Allaah Amesema,
“ Enyi mlio amini! Mcheni Allaah kama ipasavyo kumcha; wala msife ila nanyi ni Waislamu.” (Aal 'Imraan 3:102)
Uchaji Allaah ni dalili ya iymaan. Kwani kwa uchaji Allaah ndipo mtu anaweza kudumu katika njia iliyonyooka (iliyo sawa).
Jueni kuwa muongozo sahihi ni muongozo wa Muhammad (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam), Ubaya wa mambo yote ni uzushi, na kila uzushi ni uovu, na kila ovu linampeleka mtu motoni.
Enyi Waislamu! Allaah Amewaumba viume ili wamuabudu na wafungamane na Amri Zake na makatazo Yake. Allaah Anasema,
"Nami Sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi." (Adh-Dhaariyaat 51:56)
Allaah pia Anasema,
"Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Aliyekuumbeni nyinyi na wale wa kabla yenu, ili mpate kuokoka." (Al-Baqarah 2:21)
Mitume
(‘Alayhimus Salaam) hawakutumwa, wala Vitabu havikuteremshwa, wala Pepo
na Moto havikuumbwa ila kwa ukweli huu mtukufu, wa kuwatoa watu kutoka
kuabudu matamanio yao na kuwaleta katika kumuabudu Muumba wao Peke Yake.
Wametakiwa kuamini upwekwe Wake, kutekeleza amri Zake na kujiepusha na
makatazo Yake katika vipengele vyote vya maisha. Wameamrishwa pia
kurejea katika sharia Zake katika mambo yote na kujisalimisha katika
maamuzi Yake katika hali zote. Vitabu vya Allaah na Sunnah za Mtume Wake
(Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam)
kwa pamoja vinakusudia lengo hili, ili mtu aweze kufanya matendo yale
tu yanayomridhia Allaah. Iwapo mtu atakwenda kinyume na lengo hili,
anatahadharishwa na adhabu hapa duniani na kesho Akhera. Allaah
Anasema,
“
Jueni kuwa hakika ni vya Allaah vilivyomo mbinguni na ardhini. Hakika
Yeye Anajua mlionayo. Na siku mtakaporudishwa Kwake Atawaeleza
waliyoyafanya. Na Allaah ni Mjuzi wa kila kitu.” (An-Nuur 24:63)
Ndugu katika iymaan! Msingi wa kumuasi Allaah ni kufuata matamanio na kujisalimisha na matamanio ya kupita na starehe za muda. Allaah Anahesabu kufuata matamanio kuwa ni kinyume cha uongofu. Anasema,
” Je! Tuwafanye walioamini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au Tuwafanye wachaji Allaah kama waovu?.” (Swaad 38:28)
Na Akasema,
"Basi ama yule aliye zidi ujeuri"
"Na akakhiari maisha ya dunia"
” Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
"Na ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, na akajizuilia nafsi yake na matamanio"
"Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!”
(An-Naazi’aat 79:37-41)
Allah pia Anasema kuhusu Mtume Wake (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam),
"Wala hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni ufunuo uliofunuliwa" (An-Najm 53:3-4)
Inajulikana
kutokana na uzoefu na ushahidi wa maandishi kuwa faida za dunia hii na
zile za Akhera haziwezi kupatikana kwa kufuata matamanio na
kujisalimisha na shauku bila kizuizi chochote. Kufanya hivyo kunapelekea
machafuko (sheria mkononi), mauaji, vita na maangamizi.
Enyi Waislam! Hakuwezi kuwa na Uislamu wa kweli iwapo akili hazitojisalimisha na kukubali kikamilifu matakwa ya Allaah. Na Allah Anasema,
"Sema:
Hakika Sala yangu, na ibada zangu, na uhai wangu, na kufa kwangu, ni
kwa ajili ya Allaah, Mola wa viumbe vyote. Hana mshirika wake. Na hayo
ndiyo niliyoamrishwa, na mimi ni wa kwanza wa Waislamu." (Al-An'aam 6:162-163)
Asili
ya Uislam ni kujisalimisha kwa Allaah kwa utii, ina maana kusiwe na
mashaka yoyote na kukubali kwa kuridhia maamuzi Yake na amri Zake katika
vipengele vyote vya maisha. Huu ndio msingi wa Uislam. Yeyote
atakaepinga sharia za Allaah kwa maoni yake hakujisalimisha kwa Allaah.
Yeye ni mtumwa tu wa matamanio yake, na yeye ndie yule aliyetajwa kwa
maneno ya Allaah,
”
Je! Umemwona aliyefanya matamanio yake kuwa ndiye mungu wake, na Allaah
Akamwacha apotee pamoja na kuwa ana ujuzi, na akapiga muhuri juu ya
masikio yake, na moyo wake, na Akambandika vitanga machoni mwake? Basi
nani atamwongoa huyo baada ya Allaah? Hamkumbuki?” (Al-Jaathiyah 45:23)
Allah pia anasema,
"Na
ikiwa hawakuitikii, basi jua kuwa wanafuata pumbao lao tu. Na nani
aliyepotea zaidi kumshinda anayefuata pumbao lake bila ya uongofu utokao
kwa Allaah. Hakika Allaah Hawaongoi watu wenye kudhulumu." (Al-Qasas 28:50)
Kujisalimisha
katika matakwa ya Allaah katika mambo yote si msingi tu wa Uislam; bali
pia ni sharti la iymaan ya kweli. Allaah Anasema,
"La!
Naapa kwa Mola wako! Hawatoamini mpaka wakufanye wewe ndiye muamuzi
katika yale wanayokhitalifiana, kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu
ya hukumu utayotoa, na wanyenyekee kabisa." (An-Nisaa 4:65)
Katika hadiyth, Mtume wa Allaah (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam) anasema, “Hatoamini mmoja wenu hadi yawe matamanio yake ni yale niliyokuja nayo”
Enyi
Waislam! Ingawa sharia za Kiislam na kanuni zake zinawafikiana na
mahitaji ya binaadamu, sharia hizi hazitegemei shauku na matamanio ya
binaadamu. Allaah anasema,
"Na
lau kuwa Haki ingelifuata matamanio yao, basi zingeliharibika mbingu na
ardhi na waliomo ndani. Bali tumewaletea ukumbusho wao, nao wanajitenga
mbali na ukumbusho wao." (Al-Mu-minuun 23:71)
Shaykhul-Islaam ibn Taymiyyah anasema, “Ni
Kitabu tu kotuka mbinguni kinachoweza kutatua matatizo ya watu. Lau
kama watu wangeachwa kufuata rai zao, basi kila mmoja kati yao bila
shaka angekuwa na rai”
Ndugu
wapenzi! Muislamu anaweza kuwa dhaifu, akampa shetani fursa ya
kumlazimisha kufanya madhambi. Iwapo atatubia kutokana na madhambi hayo,
Allaah Atamkubalia toba yake; lakini iwapo atakufa kabla ya kutubia
Allaah Anaweza Akampa adhabu Akitaka au Akamsamehe Akitaka. Hii ni hali
ya watu karibu wote. Wana Adam wote ni wafanya madhambi na waliobora
katika wafanya madhambi ni wale wenye kutubia.
Mtu
wa kulaumiwa anayestahiki tishio la adhabu ni yule mwenye majivuno,
anayejadili kwa kukubaliana na madhambi na matamanio yake, anayepinga
makatazo ya Allaah kwa maoni yake, anakusudia kuudhalilisha Uislam,
anapiga vita akhlaaq zote zinazokwenda kinyume na matamanio yake na
kukubaliana na mambo yote yanayopendzesha matamanio yake tu.
Mtu huyu anafuata njia za wanafilosofia wa zamani kwa kukubaliana na
anayoyataka na asiyoyataka tu katika matamanio yake mpaka akapotea
katika giza la starehe na makosa, kama chombo kilichochanganyikiwa, hakitambui kipi kilicho kizuri au kukataa kilicho kibaya.
Shaykhul-Islaam ibn Taymiyyah amesema, “Kufuata matamanio katika masuala ya dini ni kubaya zaidi kuliko kufuata mambo mengine ya starehe Hiyo
ya mwanzo ilikuwa ndio hali ya wasioamini miongoni mwa washirikina.
Hawa ndio wale waliokusudiwa na maneno ya Mtume katika hadiyth
iliyosimuliwa na Hudhayfah,
“Kutakuwa na watu katika milango ya moto watakaowaita watu kuingia
humo. Atakayeitikia wito wao, basi watamtupa kwenye moto. Nikasema, “Ee
Mtume wa Allaah, tujulishe kuhusu watu hao. Akasema: Sawa. Hao ni watu
katika sisi na wanaozungumza lugha yetu.”
Mtume wa Allaah (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam) pia amesema, “Watu
watazuka kutoka katika umma wangu ambao watakuwa wamejaa matamanio kama
ugonjwa wa kuambukizwa na mnyama unavyozagaa mwili mzima na kuathiri
mishipa na viungo vyote” Abu Dawuud
Ash-Shaatwibiy amesema, “
Kile wanachofanya ni kuwa wanafuata hukumu za akili zao tu na
kushirikisha hayo na sheria za Allaah katika kukubaliana au
kutokubaliana na jambo. Iwapo wangesita hapo, mambo yangekuwa ni mepesi
zaidi bali wamekiuka mipaka yote mpaka wakatangaza vita dhidi ya Allaah
na Mtume Wake (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam) kwa kukipinga kitabu cha Allaah na Sunnah za Mtume Wake.”
Enyi
Waislamu! Hakuna nafasi kwa akili ya mtu binafsi mbele ya ushahidi wa
maandiko, na kunatakiwa kusiangaliwe mawazo ya yeyote mbele ya maamuzi
ya Allaah na yale ya Mtume Wake. Allaah anasema,
"Haiwi
kwa Muumini mwanamume wala Muumini mwanamke kuwa na khiari katika
jambo, Allaah na Mtume wake wanapokata shauri katika jambo lao. Na
mwenye kumuasi Allaah na Mtume wake basi hakika amepotea upotofu ulio
wazi." (Al-Ahzaab 33:36)
Kuonyesha kuchukizwa na sheria ya Allaah na kutafuta sheria nyingine kinyume na Zake kunafisidi amali. Allaah Anasema:
"Hayo ni kwa sababu waliyachukia Aliyoyateremsha Allaah, basi Akaviangusha vitendo vyao." (Muhammad 47:9)
Ibn Rajab anasema, “Madhambi yanafanywa kwa sababu ya kupendelea matamanio zaidi kuliko mapenzi ya Allaah na Mtume Wake (Swalla Allahu ‘alayhi wa sallam).
Uzushi katika dini ni matokeo ya kupendelea matamanio zaidi kuliko
sheria za Allaah, na hii ni hatari zaidi. Iwapo akili imeshazoeshwa
matamanio, kuitoa akili hiyo nje ya matamanio ni kugumu."
Ndugu
katika Iymaan! Allaah Ameumba mipaka katika uwezo wa akili ya
binaadamu. Haiwezekani kwa akili ya binaandamu kufahamu kila kitu kwa
usahihi wake. Ujuzi wa kila kitu ni sifa maalumu ya Allaah Peke Yake.
Ufahamu wa binaadamu una kasoro na (binaadam) hawawezi kukubaliana na
nadharia yoyote. Ndio sababu ukawaona wanaanza kufuata mawazo/rai fulani
leo na wanaachana nayo kesho na kufuata mtazamo mwengine, na kesho
kutwa wanahamia katika rai nyingine tofauti. Iwapo kila maamuzi yanayochukuliwa
kwa akili za binaadamu ni sahihi kungekuwa na uhakika wa kutosha wa
maisha mazuri ya watu wote katika dunia yao na Akhera yao, kusingekuwa
na haja ya kutumwa Mitume na kusingekuwa na haja ya ujumbe mtukufu.
Imekuwa
kwa hivyo ni lazima kwa Muislam kuwa macho katika kufuata njia ya
hatari yenye makosa ya kukataa sehemu yoyote ya maamrisho ya Allaah na
kuchukizwa nayo au kupendelea zaidi matamanio na kujadili juu ya Sharia
(Ya Allaah). Wafuasi wa Sunnah wamekubaliana ya kuwa yeyote anayefanya
mambo yaliyokatazwa ambayo yako chini ya ushirikina, basi mtu huyo
atachukuliwa kuwa hakuamini; na yeyote ataeyachukulia mambo
yaliyokatazwa kuwa yanafaa – hata kama hayafanyi- mtu huyo hakuamini,
iwapo mambo hayo yanaangukia katika mambo ambayo ni lazima yajulikane
katika dini.
Waache wale wanaotafuta uongofu wasome maneno ya Allaah kwamba,
"Na
kwa hakika hii ndiyo Njia yangu Iliyo Nyooka. Basi ifuateni, wala
msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake. Haya amekuusieni ili
mpate kumcha Allaah." (Al-An'aam 6:153)
Enyi
Waislamu! Mazingatio yamesifiwa kwa binaadamu. Kama si hivyo,
kusingekuwa ni wajibu ulioamrishwa maalum juu ya binaadam. Allaah
Ameelezea mazingatio ya binaadamu katika aya nyingi katika Kitabu Chake.
Amemuamrisha binaadamu kufikiri na kufahamu. Yeye pia amefahamisha
sababu mbali mbali katika Amri Zake nyingi Anamalizia kwa Kusema, “ Ili mpate kufahamu”.
Ingawa
ni Allaah Mwenyewe Aliyeumba ufahamu kwa binaadamu, Amewafanya tofauti
baina mmoja na mwengine. Ameumba hisia na matamanio ya kimaumbile ya
binaadamu lakini Akaifanya Sharia iwe ni hakimu wa yote hayo, Yeye
(Allaah) Anaweza kumuweka mtu katika mtihani. Yule atakayejisalimisha
kwa Allaah peke yake ndie Muislam wa kweli ambaye anamtii Allaah na kwa
hivyo, anastahiki Pepo. Lakini yule anayejivuna na akatumia akili na
kuasi amri za Allaah, yeye ameahidiwa adhabu.
Wanachuoni
wametaja tabia za watu wa matamanio na wale waliopendelea zaidi maoni
yao juu ya Sheria sahihi za Kiislam na amri zake. Kuwa tabia hizi
zilikuwepo kwa watu wa matamanio wa umma za mwamzo, na vile vile zipo
kwa ummah wa mwisho. Moja ya tabia hizi ni kufuata aya zisizo wazi (mutashaabihaati) katika Qur’aan. Allaah Anasema,
"Yeye
ndiye Aliyekuteremshia Kitabu hichi. Ndani yake zimo Aaya muhkam, zenye
maana wazi. Hizo ndizo msingi wa Kitabu hichi. Na ziko nyengine za
mifano. Ama wale ambao nyoyoni mwao umo upotovu wanafuata zile za mifano
kwa kutafuta fitna, na kutafuta maana yake; na wala hapana ajuaye maana
yake ila Allaah. Na wale wenye msingi madhubuti katika ilimu husema:
Sisi tumeziamini, zote zimetoka kwa Mola wetu . Lakini hawakumbuki hayo
isipokuwa wenye akili." (Aal 'Imraan 3:7)
Tabia
nyingine ya watu hawa ni kuwa wanawatukana Waislam wa mwanzo, kama
Maswahaba ambao wanajulikana (ni maarufu) kwa elimu yao na uchaji
Allaah wao na wameigwa na wale waliokuja baada yao. Watu wa matamanio
wanawasifu wale wanaokubaliana na shauku zao kama wanafalsafa.
Watu
wa matamanio pia wanajulikana kwa kudharau amri za Uislam na kutojali
kwao katika kuzipinga. Baadhi yao hata wamefikia kiwango cha kuzifanyia
mzaha amri hizi na kuwafanyia mzaha wale waliofungamana na amri hizo na
kuwatoa makosa na kuwalaumu.
Tabia
nyingine ya watu wa matamanio ni kuwa wao hawafuati Sunnah katika
matendo yao ya ibada, desturi zao na hali zao. Pamoja na hayo, utamuona
mmoja wao akijifananisha na wanachuoni watukufu/maarufu wa Sunnah. Wao ni kama wale Allaah Aliowaeleza katika Qur-aan kama,
"Na katika watu wapo wanaobishana juu ya Allaah bila ya elimu, wala uongofu, wala Kitabu chenye nuru. Anayegeuza
shingo yake ili kupoteza watu waache Njia ya Allaah. Duniani atapata
hizaya, na Siku ya Qiyaama Tutamwonjesha adhabu ya kuungua. (Ataambiwa):
Hayo ni kwa sababu ya iliyotanguliza mikono yako. Na hakika Allaah si
dhaalimu kwa waja.” (Al-Hajj 22:8-10)
Ya Allaah! Zithibitishe nyoyo zetu katika dini na uwaongoze wale Waislamu waliokwenda upande.
»
|
Yanayohusiana
FeatureZingatioNyumba Ya Aakhirah Umeshaijenga?
Miongoni
mwa nguzo za iymaan ni kuamini kwamba kuna hesabu Siku ya Qiyaamah.
Hesabu ambayo itamtambua kwamba ni mtu wa Peponi ama ni motoni. Mola
Atujaalie kuwa miongoni mwa watu wa Peponi, Aamiyn.
|
|
welcm
ReplyDeleteall