UMUHIMU WA.............

Kwa kuwa blog yako ya ANGAZA inapenda kuangaza na wewe hivyo inapenda kukuuliza wewe kama mdau wetu ""UNADHANI KUNA UMUHIMU WA KUWARUHUSU WANAFUNZI KUMILIKI SIMU SHULENI????

Tunatumai kila mmoja atakuwa na hoja kulingana na yeye anavyouona umuhimu wa kumiliki simu hasa hasa tukizungumzia juu ya WANAFUNZI hapo tunaweza kupata hoja tofauti tofauti huku wengine wakidiliki kusema kuwa SIMU zinawarahisishia kusoma na kupata taarifa kwa urahisi!!! Lakini tukiliangalia suala hili kwa umakini tutagundua mengi yanayo wafanya wanafunzi kuwa na matumizi tofauti na yale ambayo wao uyajibu pindi waulizwapo juu ya umuhimu wa kutumia SIMU. Moja ya kuyapata majibu ya matumizi ya simu za wanafunzi tunaweza kuyapata kwa kuitumia mitndao ya kijamii hasa hasa hii
  • FACEBOOK
  • WHATSAPP
  • INSTGRAM
  • TWITTER n.k hapo utagundua majibu ya matumizi ya SIMU kwa wanafunzi ngazi zote yaani kuanzia SHULE ZA MISINGI, SEKONDARI na VYUONI. Kwa mara nyingi ukifuatilia baadhi ya mitandao hii ya kijamii kwanza ni ukweli usiopingika kuwa wanafunzi ni wengi katika mitandao hii ya kijamii kuliko watumiaji wasio wa mashuleni. Na ukiendelea kufuatilia juu ya post zao utahisi kampeni za SODOMA na GOMOLA tayari zimeanza. Hivyo wewe kama ni mwanafunzi tafadhali iepuke fitina ya mnyama (666) kwa kuitumia simu yako kwenye mambo muhimu ya maana na sio kwenye mambo machafu"" Japokuwa watakupa laini yenye vifurushi vya kipekee lakini chonde chonde itumie kwa kujistili na sio ufurahi kwa vile unaweka kiasi kidogo cha malipo na unapewa MB nyingi nawe uanze kuhutumia mtandao ndivyo sivyo.  Katika pita pita yetu ANGAZA iliweza kufanya utafiti shule moja iliyoko nchini UGANDA  shule hiyo inawafundisha wanafunzi kupitia mtandaoni (online) Lakini tuligundua kuwa kati ya wanafunzi 20 wanaokuwa (online) ni wanafunzi 4 wanokuwa tayari kujibu kwa wakati husika na wanafunzi 6 wanakuwa online YOUTUBE wakiangalia video chafu (ngono) na wanafunzi 10 wanakuwa (online) FACEBOOK wakichati. 
  • Hivyo ni kilio kikubwa juu ya wanafunzi na wale wote wasiokuwa wanafunzi maana wao wanashangilia na kuliona ni jambo la kheri kuwepo kwa mitandao ya kijamii lakini hawajui kuwa ni moja kati ya fitina za mnyama (666) Uwezi amini kwa sasa mtoto yuko FACEBOOK, na baba yuko FACEBOOK na mtoto anapost picha kavaa vimini nusu uchi alafu ukiangalia kwenye majina ya wale walio LIKE ile picha na baba yake yumo katika list hiyo.  haishii hapo wewe ukitaka kujua kuwa fitina ya mnyama (666) inazidi kuenea ebu ichukue simu ya mwanafunzi kisha ifungue ndani ikague'' usipokutana na picha za maajabu basi video zitakutoa jasho.**********************************************************************
  • ********************AnGaNzA*****************ANGAZA**************************** 

Share on Google Plus

About DAIMA ANGAZA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

1 comments: