Hadiyth La Wiki
Hadiyth Al-Qudsiy Hadiyth Ya 42: Watu Wa Jannah Watapata Ridhaa Ya Allaah
عَنْ
أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ
عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((إِنَّ اللَّهَ تَبَارَكَ وَتَعَالَى يَقُولُ
لِأَهْلِ الْجَنَّةِ: يَا أَهْلَ الْجَنَّةِ! فَيَقُولُونَ لَبَّيْكَ رَبَّنَا وَسَعْدَيْكَ، فَيَقُولُ: هَلْ رَضِيتُمْ؟ فَيَقُولُونَ وَمَا لَنَا لَا نَرْضَى وَقَدْ أَعْطَيْتَنَا مَا لَمْ تُعْطِ أَحَدًا مِنْ خَلْقِكَ، فَيَقُولُ: أَنَا أُعْطِيكُمْ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ،
قَالُوا: يَا رَبِّ وَأَيُّ شَيْءٍ أَفْضَلُ مِنْ ذَلِكَ؟ فَيَقُولُ:
أُحِلُّ عَلَيْكُمْ رِضْوَانِي فَلَا أَسْخَطُ عَلَيْكُمْ بَعْدَهُ
أَبَدًا)) البخاري، مسلم و الترمذي
Imepokelewa kutoka kwa
Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah
(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: (Allaah Tabaaraka wa Ta’aalaa Atawaambia
watu wa Jannah: Enyi watu wa Jannah! Watasema: Labeka Rabb wetu tuko
chini ya amri Yako na kheri zote zimo katika Mikono Yako. Kisha Atasema:
Je,
mmeridhika? Watasema: Vipi tusiridhike na hali Umetupa ambayo Hukumpa
yeyote mwengine katika viumbe Vyako? Kisha Atasema: Nitakupeni kilicho
bora kuliko hayo. Watasema: Ee Rabb, ni kipi kilicho bora kuliko haya?
Atasema: Nitafanya ridhaa (mapenzi) Yangu iwateremkie na baada ya hapo
Sitoghadhibika nanyi tena abadan) [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhy]
إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ -Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada:Kutawasali Kwa Du'aa Ya Nabiy Yuwnus
إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ
Wewe Pekee Tunakuabudu
Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada
Tawassul Zinazokubalika Katika Shariy’ah
Kutawasali Kwa Du'aa Ya Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam)
Du'aa
ya Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam) ni sababu mojawapo kubwa ya kuitikiwa
du’aa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Nabiy Yuwnus
('Alayhis-Salaam) baada ya kuwalingania watu wake katika Tawhiyd
wakakanusha, aliwakimbia bila ya kupata idhini ya Allaah (Subhaanahu wa
Ta'aalaa) hivyo akamkosea Rabb Wake. Baada ya kutupwa baharini kutoka
katika jahazi aliyoipanda kwa ajili ya kukimbia mbali, Allaah
(Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akamuamrisha nyangumi ammeze bila ya kumla
nyama yake au kumvunja mifupa yake. Akabakia tumboni mwa nyangumi kwa
masiku kadhaa, akawa anaomba du’aa hiyo ya kujirudi kwa Rabb Wake.
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:
وَذَا
النُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَاضِبًا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقْدِرَ عَلَيْهِ
فَنَادَىٰ فِي الظُّلُمَاتِ أَن لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ
إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٧﴾
Na
Dhan-Nuwn (Yuwnus) alipoondoka akiwa ameghadhibika, akadhani kwamba
Hatutamdhikisha; akaita katika kiza kwamba: “Hapana muabudiwa wa haki
isipokuwa Wewe, Utakasifu ni Wako, hakika mimi nilikuwa miongoni mwa
madhalimu.” [Al-Anbiyaa: 87]
Basi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akamtakabalia:
فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَنَجَّيْنَاهُ مِنَ الْغَمِّ ۚ وَكَذَٰلِكَ نُنجِي الْمُؤْمِنِينَ ﴿٨٨﴾
Basi Tukamuitikia na Tukamuokoa kutokana na ghamu. Na hivyo ndivyo Tuwaokoavyo Waumini. [Al-Anbiyaa: 88]
Na
Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akathibitisha kwamba
du’aa hiyo aliyoiomba Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam) ni du’aa
inayosababisha kutakabaliwa du’aa:
عَنْ
سَعْدٍ بن أبي وقاص (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ
(صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ: ((دَعْوَةُ ذِي النُّونِ إِذْ دَعَا
وَهُوَ فِي بَطْنِ الْحُوتِ: "لاَ إِلَهَ إلاَّ أَنْتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي
كُنْتُ مِنْ الظَّالِمِينَ" فَإِنَّهُ لَمْ يَدْعُ بِهَا رَجُلٌ مُسْلِمٌ
فِي شَيْءٍ قَطُّ إِلاَّ اسْتَجَابَ اللَّهُ لَهُ))
Kutoka
kwa Sa’d bin Abi Waqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa
Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Du’aa ya
Dhan-Nuwn (Nabiy Yuwnus 'Alayhis Salaam) alipoomba alipokuwa katika
tumbo la nyangumi:
“Laa ilaaha illa Anta Subhaanaka inniy kuntu minadhw-dhwaalimiyn”
basi hakika hakuna Muislamu aombaye kwayo kitu chochote kile ila Allaah Atamuitikia)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3505), Swahiyh Al-Jaami’ (3383), Takhriyj Al-Mishkaat Al-Maswaabiyh (2232), As-Silsilah Asw-Swahiyhah (1744)]
Bila
ya shaka du’aa ya Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam) inastahiki kuwa ni
wasiylah ya kutakabaliwa du’aa kwa sababu du’aa hiyo imegawanyika
katika sehemu tatu:
1. Kumpwekesha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
لاَ إِلَهَ إلاَّ أَنْتَ
Hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Wewe.
Shaykhul-Islaam Ibn
Taymiyyah amesema: “(Nabiy Yuwnus ‘Alayhis-Salaam) Amekiri Tawhiyd ya
Uluwhiyyah ambayo inahusiana na aina mojawapo ya du’aa (Du’aa ya
‘ibaadah) kwa sababu ‘Ilaah’ Ndiye Mwenye kustahiki kuombwa aina zote
mbili za du’aa; du’aa ya ‘ibaadah na du’aa ya mas-alah (jambo). Naye
Ndiye Allaah Hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Yeye.” [Kuulizwa kwake
Shaykh kuhusu du’aa ya Dhan-Nuwn]
2. Kumsabbih (kumtakasa) Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):
سُبْحَانَكَ
Utakasifu ni Wako.
3. Kukiri madhambi
إِنِّي كُنْتُ مِنْ الظَّالِمِينَ
Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu.
Akasema tena Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah: “Kuhusu kauli yake: “Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu” Inahusiana na kukiri kwake dhambi, na hivyo ni kuomba maghfirah.”
Na Istighfaar (kuomba maghfirah) kuna faida tele kwa dalili kadhaa.
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)
اسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ إِنَّهُ كَانَ غَفَّارًا ﴿١٠﴾
Ombeni maghfirah kwa Rabb wenu; hakika Yeye ni Mwingi mno wa kughufuria.
يُرْسِلِ السَّمَاءَ عَلَيْكُم مِّدْرَارًا ﴿١١﴾
Atakutumieni mvua kutoka mbinguni, tele ya kuendelea.
وَيُمْدِدْكُم بِأَمْوَالٍ وَبَنِينَ وَيَجْعَل لَّكُمْ جَنَّاتٍ وَيَجْعَل لَّكُمْ أَنْهَارًا ﴿١٢﴾
Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakupeni mito. [Nuwh: 10-12]
إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ -Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada:Kutawasali Kwa Du'aa Ya Nabiy Yuwnus
إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ
Wewe Pekee Tunakuabudu
Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada
Tawassul Zinazokubalika Katika Shariy’ah
Kutawasali Kwa Du'aa Ya Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam)
Du'aa
ya Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam) ni sababu mojawapo kubwa ya kuitikiwa
du’aa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Nabiy Yuwnus
('Alayhis-Salaam) baada ya kuwalingania watu wake katika Tawhiyd
wakakanusha, aliwakimbia bila ya kupata idhini ya Allaah (Subhaanahu wa
Ta'aalaa) hivyo akamkosea Rabb Wake. Baada ya kutupwa baharini kutoka
katika jahazi aliyoipanda kwa ajili ya kukimbia mbali, Allaah
(Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akamuamrisha nyangumi ammeze bila ya kumla
nyama yake au kumvunja mifupa yake. Akabakia tumboni mwa nyangumi kwa
masiku kadhaa, akawa anaomba du’aa hiyo ya kujirudi kwa Rabb Wake.
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:
وَذَا
النُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَاضِبًا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقْدِرَ عَلَيْهِ
فَنَادَىٰ فِي الظُّلُمَاتِ أَن لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ
إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٧﴾
Na
Dhan-Nuwn (Yuwnus) alipoondoka akiwa ameghadhibika, akadhani kwamba
Hatutamdhikisha; akaita katika kiza kwamba: “Hapana muabudiwa wa haki
isipokuwa Wewe, Utakasifu ni Wako, hakika mimi nilikuwa miongoni mwa
madhalimu.” [Al-Anbiyaa: 87]
Basi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Akamtakabalia:
فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَنَجَّيْنَاهُ مِنَ الْغَمِّ ۚ وَكَذَٰلِكَ نُنجِي الْمُؤْمِنِينَ ﴿٨٨﴾
Basi Tukamuitikia na Tukamuokoa kutokana na ghamu. Na hivyo ndivyo Tuwaokoavyo Waumini. [Al-Anbiyaa: 88]
Na
Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akathibitisha kwamba
du’aa hiyo aliyoiomba Nabiy Yuwnus ('Alayhis-Salaam) ni du’aa
inayosababisha kutakabaliwa du’aa:
عَنْ
سَعْدٍ بن أبي وقاص (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ
(صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ: ((دَعْوَةُ ذِي النُّونِ إِذْ دَعَا
وَهُوَ فِي بَطْنِ الْحُوتِ: "لاَ إِلَهَ إلاَّ أَنْتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي
كُنْتُ مِنْ الظَّالِمِينَ" فَإِنَّهُ لَمْ يَدْعُ بِهَا رَجُلٌ مُسْلِمٌ
فِي شَيْءٍ قَطُّ إِلاَّ اسْتَجَابَ اللَّهُ لَهُ))
Kutoka
kwa Sa’d bin Abi Waqaasw (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa
Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Du’aa ya
Dhan-Nuwn (Nabiy Yuwnus 'Alayhis Salaam) alipoomba alipokuwa katika
tumbo la nyangumi:
“Laa ilaaha illa Anta Subhaanaka inniy kuntu minadhw-dhwaalimiyn”
basi hakika hakuna Muislamu aombaye kwayo kitu chochote kile ila Allaah Atamuitikia)) [Swahiyh At-Tirmidhiy (3505), Swahiyh Al-Jaami’ (3383), Takhriyj Al-Mishkaat Al-Maswaabiyh (2232), As-Silsilah Asw-Swahiyhah (1744)]
0 comments:
Post a Comment