DIAMOND PLATNUMZ AZIDI KUWAVUTA VIJANA SHANGWE LA SHETANI

Hakuna anayeweza kupinga kwamba mara nyingi wasanii wamekuwa wakidai kuwa wao ni vioo vya jamii yaani wakiwa na maana kuwa Jamii inabidi iige kwao na nkujifunza kwao vilevile. Na hii imepelekea vijana wengi kupotea njia na kuanza kuyafanya yaliyo tofauti sana na makusudio ya wao kuumbwa na kuwepo hapa duniani. Ni wazi kuwa Mwenyezi Mungu alipo muumba mwanadamu yaani Adam ilikuwa kwamba yeye na kizazi chake chote kimfanyie ibada Mwenyezi Mungu kwa kumsujudia yeye, Kumuomba msaada yeye, Kumpwekesha yeye kwa kila hari kwa kila jambo pia. Lakini pia ni wazi kuwa vilevile Shetani alipo alipo hukumiwa na kufukuzwa na kutelemshwa Dunia aliapa kuwa ataakikisha yeye atakipotosha kizazi cha Adam ili apate kuingia nacho motoni'''' Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni mwingi wa rehema akukiacha kizazi cha Adam kiangaike na kikose msaada ndipo akasema hakika nitawatumia viongozi wa kuwajulisha kuwa Shetani ni adui yenu na yeyote mwenye kumfuata ataingia naye motoni......hapa ndipo Mwenyezi Mungu alipo anza kuwaleta Mitume na Manabii ili kila Mwenye kuwaamini anusulike na moto wa Jehanamu ambao usababishwa na Shetani. Sasa tazama Shetani amekuwa mwenye kuwapambia wanadamu kulingana na matamanio ya nafsi zao leo hii utasikia vijana wanafanya mziki kuwa ajira na wengine wakiamini kuwa mchezaji ni salama kwao"''"'Lakini shetani hajaishia hapo akawafanya wana wa Adam waamini kuwa ukifanya mapenzi sio tatizo na ukipata riba kutoka kwa unayemdai hakuna shida!!!!! Vilevile shetani akazidi kumpambia mwana wa Adam kuwa akiabudu masanamu hakuna shida!! Lakini tazama Wasanii wamedumbukia katika janga hili la kumtukuza Shatani na kuwafanya wanaowatizama nao wadhanie kuwa wako salama kumbe wanavutwa na Shetani.....na ndio maana kampeni zinazidi kufanyika mara utasikia kuna maswala ya FIESTA, DANCE MIA 100,,MTV, n.k na tizama wanajamii wamecopy hayo na kujikuta list inazidi kuwa kubwa ya kumwimbia shetani na kumshangilia bila ya kujua kuwa huko ndiko kuangamia na mwisho kutiwa motoni. 
Share on Google Plus

About DAIMA ANGAZA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment